النجم   سورة  : An-Najm


سورة Sura   النجم   An-Najm
وَأَنَّهُ خَلَقَ الزَّوْجَيْنِ الذَّكَرَ وَالْأُنثَىٰ (45) مِن نُّطْفَةٍ إِذَا تُمْنَىٰ (46) وَأَنَّ عَلَيْهِ النَّشْأَةَ الْأُخْرَىٰ (47) وَأَنَّهُ هُوَ أَغْنَىٰ وَأَقْنَىٰ (48) وَأَنَّهُ هُوَ رَبُّ الشِّعْرَىٰ (49) وَأَنَّهُ أَهْلَكَ عَادًا الْأُولَىٰ (50) وَثَمُودَ فَمَا أَبْقَىٰ (51) وَقَوْمَ نُوحٍ مِّن قَبْلُ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا هُمْ أَظْلَمَ وَأَطْغَىٰ (52) وَالْمُؤْتَفِكَةَ أَهْوَىٰ (53) فَغَشَّاهَا مَا غَشَّىٰ (54) فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكَ تَتَمَارَىٰ (55) هَٰذَا نَذِيرٌ مِّنَ النُّذُرِ الْأُولَىٰ (56) أَزِفَتِ الْآزِفَةُ (57) لَيْسَ لَهَا مِن دُونِ اللَّهِ كَاشِفَةٌ (58) أَفَمِنْ هَٰذَا الْحَدِيثِ تَعْجَبُونَ (59) وَتَضْحَكُونَ وَلَا تَبْكُونَ (60) وَأَنتُمْ سَامِدُونَ (61) فَاسْجُدُوا لِلَّهِ وَاعْبُدُوا ۩ (62)
القمر Al-Qamar
اقْتَرَبَتِ السَّاعَةُ وَانشَقَّ الْقَمَرُ (1) وَإِن يَرَوْا آيَةً يُعْرِضُوا وَيَقُولُوا سِحْرٌ مُّسْتَمِرٌّ (2) وَكَذَّبُوا وَاتَّبَعُوا أَهْوَاءَهُمْ ۚ وَكُلُّ أَمْرٍ مُّسْتَقِرٌّ (3) وَلَقَدْ جَاءَهُم مِّنَ الْأَنبَاءِ مَا فِيهِ مُزْدَجَرٌ (4) حِكْمَةٌ بَالِغَةٌ ۖ فَمَا تُغْنِ النُّذُرُ (5) فَتَوَلَّ عَنْهُمْ ۘ يَوْمَ يَدْعُ الدَّاعِ إِلَىٰ شَيْءٍ نُّكُرٍ (6)
الصفحة Page 528
(45) Na kwamba Yeye ndiye aliye umba jozi, dume na jike
(46) Kutokana na mbegu ya uzazi inapo miminwa.
(47) Na kwamba ni juu yake ufufuo mwengine.
(48) Na kwamba ni Yeye ndiye anaye tosheleza na kukinaisha.
(49) Na kwamba hakika Yeye ndiye Mola Mlezi wa nyota ya Shii'ra.
(50) Na kwamba Yeye ndiye aliye waangamiza A'di wa kwanza,
(51) Na Thamudi hakuwabakisha,
(52) Na kabla yao kaumu ya Nuhu. Na hao hakika walikuwa ni madhaalimu zaidi, na waovu zaidi;
(53) Na miji iliyo pinduliwa, ni Yeye aliye ipindua.
(54) Vikaifunika vilivyo funika.
(55) Basi neema gani ya Mola wako Mlezi unayo ifanyia shaka?
(56) Hili ni Onyo katika maonyo yale yale ya zamani.
(57) Kiyama kimekaribia!
(58) Hapana wa kukifichua isipo kuwa Mwenyezi Mungu.
(59) Je! Mnayastaajabia maneno haya?
(60) Na mnacheka, wala hamlii?
(61) Nanyi mmeghafilika?
(62) Basi msujudieni Mwenyezi Mungu, na mumuabudu.
القمر Al-Qamar
(1) Saa imekaribia, na mwezi umepasuka!
(2) Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea.
(3) Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti.
(4) Na bila ya shaka zimewajia khabari zenye makaripio.
(5) Hikima kaamili; lakini maonyo hayafai kitu!
(6) Basi jiepushe nao. Siku atakapo ita mwitaji kuliendea jambo linalo chusha;
 


اتصل بنا | الملكية الفكرية DCMA | سياسة الخصوصية | Privacy Policy | قيوم المستخدم

آيــــات - القرآن الكريم


© 2022