المعارج   سورة  : Al-Ma'aarij


سورة Sura   المعارج   Al-Ma'aarij
يُبَصَّرُونَهُمْ ۚ يَوَدُّ الْمُجْرِمُ لَوْ يَفْتَدِي مِنْ عَذَابِ يَوْمِئِذٍ بِبَنِيهِ (11) وَصَاحِبَتِهِ وَأَخِيهِ (12) وَفَصِيلَتِهِ الَّتِي تُؤْوِيهِ (13) وَمَن فِي الْأَرْضِ جَمِيعًا ثُمَّ يُنجِيهِ (14) كَلَّا ۖ إِنَّهَا لَظَىٰ (15) نَزَّاعَةً لِّلشَّوَىٰ (16) تَدْعُو مَنْ أَدْبَرَ وَتَوَلَّىٰ (17) وَجَمَعَ فَأَوْعَىٰ (18) ۞ إِنَّ الْإِنسَانَ خُلِقَ هَلُوعًا (19) إِذَا مَسَّهُ الشَّرُّ جَزُوعًا (20) وَإِذَا مَسَّهُ الْخَيْرُ مَنُوعًا (21) إِلَّا الْمُصَلِّينَ (22) الَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ دَائِمُونَ (23) وَالَّذِينَ فِي أَمْوَالِهِمْ حَقٌّ مَّعْلُومٌ (24) لِّلسَّائِلِ وَالْمَحْرُومِ (25) وَالَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوْمِ الدِّينِ (26) وَالَّذِينَ هُم مِّنْ عَذَابِ رَبِّهِم مُّشْفِقُونَ (27) إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمْ غَيْرُ مَأْمُونٍ (28) وَالَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَافِظُونَ (29) إِلَّا عَلَىٰ أَزْوَاجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَ (30) فَمَنِ ابْتَغَىٰ وَرَاءَ ذَٰلِكَ فَأُولَٰئِكَ هُمُ الْعَادُونَ (31) وَالَّذِينَ هُمْ لِأَمَانَاتِهِمْ وَعَهْدِهِمْ رَاعُونَ (32) وَالَّذِينَ هُم بِشَهَادَاتِهِمْ قَائِمُونَ (33) وَالَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ يُحَافِظُونَ (34) أُولَٰئِكَ فِي جَنَّاتٍ مُّكْرَمُونَ (35) فَمَالِ الَّذِينَ كَفَرُوا قِبَلَكَ مُهْطِعِينَ (36) عَنِ الْيَمِينِ وَعَنِ الشِّمَالِ عِزِينَ (37) أَيَطْمَعُ كُلُّ امْرِئٍ مِّنْهُمْ أَن يُدْخَلَ جَنَّةَ نَعِيمٍ (38) كَلَّا ۖ إِنَّا خَلَقْنَاهُم مِّمَّا يَعْلَمُونَ (39)
الصفحة Page 569
(11) Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,
(12) Na mkewe, na nduguye,
(13) Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,
(14) Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.
(15) La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,
(16) Unao babua ngozi ya kichwa!
(17) Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.
(18) Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.
(19) Hakika mtu ameumbwa na papara.
(20) Inapo mgusa shari hupapatika.
(21) Na inapo mgusa kheri huizuilia.
(22) Isipo kuwa wanao sali,
(23) Ambao wanadumisha Sala zao,
(24) Na ambao katika mali yao iko haki maalumu
(25) Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;
(26) Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,
(27) Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.
(28) Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.
(29) Na ambao wanahifadhi tupu zao.
(30) Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi -
(31) Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka.
(32) Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,
(33) Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,
(34) Na ambao wanazihifadhi Sala zao.
(35) Hao ndio watakao hishimiwa Peponi.
(36) Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu?
(37) Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!
(38) Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema?
(39) La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua.
 


اتصل بنا | الملكية الفكرية DCMA | سياسة الخصوصية | Privacy Policy | قيوم المستخدم

آيــــات - القرآن الكريم


© 2022