الانسان   سورة  : Al-Insaan


سورة Sura   الانسان   Al-Insaan
كَلَّا بَلْ تُحِبُّونَ الْعَاجِلَةَ (20) وَتَذَرُونَ الْآخِرَةَ (21) وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَّاضِرَةٌ (22) إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٌ (23) وَوُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ بَاسِرَةٌ (24) تَظُنُّ أَن يُفْعَلَ بِهَا فَاقِرَةٌ (25) كَلَّا إِذَا بَلَغَتِ التَّرَاقِيَ (26) وَقِيلَ مَنْ ۜ رَاقٍ (27) وَظَنَّ أَنَّهُ الْفِرَاقُ (28) وَالْتَفَّتِ السَّاقُ بِالسَّاقِ (29) إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ الْمَسَاقُ (30) فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ (31) وَلَٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ (32) ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰ أَهْلِهِ يَتَمَطَّىٰ (33) أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰ (34) ثُمَّ أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰ (35) أَيَحْسَبُ الْإِنسَانُ أَن يُتْرَكَ سُدًى (36) أَلَمْ يَكُ نُطْفَةً مِّن مَّنِيٍّ يُمْنَىٰ (37) ثُمَّ كَانَ عَلَقَةً فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ (38) فَجَعَلَ مِنْهُ الزَّوْجَيْنِ الذَّكَرَ وَالْأُنثَىٰ (39) أَلَيْسَ ذَٰلِكَ بِقَادِرٍ عَلَىٰ أَن يُحْيِيَ الْمَوْتَىٰ (40)
الانسان Al-Insaan
هَلْ أَتَىٰ عَلَى الْإِنسَانِ حِينٌ مِّنَ الدَّهْرِ لَمْ يَكُن شَيْئًا مَّذْكُورًا (1) إِنَّا خَلَقْنَا الْإِنسَانَ مِن نُّطْفَةٍ أَمْشَاجٍ نَّبْتَلِيهِ فَجَعَلْنَاهُ سَمِيعًا بَصِيرًا (2) إِنَّا هَدَيْنَاهُ السَّبِيلَ إِمَّا شَاكِرًا وَإِمَّا كَفُورًا (3) إِنَّا أَعْتَدْنَا لِلْكَافِرِينَ سَلَاسِلَ وَأَغْلَالًا وَسَعِيرًا (4) إِنَّ الْأَبْرَارَ يَشْرَبُونَ مِن كَأْسٍ كَانَ مِزَاجُهَا كَافُورًا (5)
الصفحة Page 578
(20) Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,
(21) Na mnaacha maisha ya Akhera.
(22) Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,
(23) Zinamwangallia Mola wao Mlezi.
(24) Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.
(25) Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.
(26) La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,
(27) Na pakasemwa: Nani wa kumganga?
(28) Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;
(29) Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,
(30) Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!
(31) Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.
(32) Bali alikanusha, na akageuka.
(33) Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.
(34) Ole wako, ole wako!
(35) Kisha Ole wako, ole wako!
(36) Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?
(37) Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?
(38) Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.
(39) Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.
(40) Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?
الانسان Al-Insaan
(1) Hakika kilimpitia binaadamu kipindi katika zama ambacho kwamba hakuwa kitu kinacho tajwa.
(2) Hakika Sisi tumemuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliyo changanyika, tumfanyie mtihani. Kwa hivyo tukamfanya mwenye kusikia, mwenye kuona.
(3) Hakika Sisi tumembainishia Njia. Ama ni mwenye kushukuru, au mwenye kukufuru.
(4) Hakika Sisi tumewaandalia makafiri minyororo na pingu na Moto mkali.
(5) Hakika watu wema watakunywa katika vinywaji vilivyo changanyika na kafuri,
 


اتصل بنا | الملكية الفكرية DCMA | سياسة الخصوصية | Privacy Policy | قيوم المستخدم

آيــــات - القرآن الكريم


© 2022