الشعراء   سورة  : Ash-Shu'araa


سورة Sura   الشعراء   Ash-Shu'araa
وَاجْعَل لِّي لِسَانَ صِدْقٍ فِي الْآخِرِينَ (84) وَاجْعَلْنِي مِن وَرَثَةِ جَنَّةِ النَّعِيمِ (85) وَاغْفِرْ لِأَبِي إِنَّهُ كَانَ مِنَ الضَّالِّينَ (86) وَلَا تُخْزِنِي يَوْمَ يُبْعَثُونَ (87) يَوْمَ لَا يَنفَعُ مَالٌ وَلَا بَنُونَ (88) إِلَّا مَنْ أَتَى اللَّهَ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ (89) وَأُزْلِفَتِ الْجَنَّةُ لِلْمُتَّقِينَ (90) وَبُرِّزَتِ الْجَحِيمُ لِلْغَاوِينَ (91) وَقِيلَ لَهُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ (92) مِن دُونِ اللَّهِ هَلْ يَنصُرُونَكُمْ أَوْ يَنتَصِرُونَ (93) فَكُبْكِبُوا فِيهَا هُمْ وَالْغَاوُونَ (94) وَجُنُودُ إِبْلِيسَ أَجْمَعُونَ (95) قَالُوا وَهُمْ فِيهَا يَخْتَصِمُونَ (96) تَاللَّهِ إِن كُنَّا لَفِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ (97) إِذْ نُسَوِّيكُم بِرَبِّ الْعَالَمِينَ (98) وَمَا أَضَلَّنَا إِلَّا الْمُجْرِمُونَ (99) فَمَا لَنَا مِن شَافِعِينَ (100) وَلَا صَدِيقٍ حَمِيمٍ (101) فَلَوْ أَنَّ لَنَا كَرَّةً فَنَكُونَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ (102) إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ (103) وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ (104) كَذَّبَتْ قَوْمُ نُوحٍ الْمُرْسَلِينَ (105) إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ (106) إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ (107) فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ (108) وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ (109) فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ (110) ۞ قَالُوا أَنُؤْمِنُ لَكَ وَاتَّبَعَكَ الْأَرْذَلُونَ (111)
الصفحة Page 371
(84) Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye.
(85) Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema.
(86) Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.
(87) Wala usinihizi Siku watapo fufuliwa.
(88) Siku ambayo kwamba mali hayato faa kitu wala wana.
(89) Isipo kuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi.
(90) Na Pepo itasogezwa kwa wachamngu.
(91) Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.
(92) Na wataambiwa: Wako wapi mlio kuwa mkiwaabudu
(93) Badala ya Mwenyezi Mungu? Je! Wanakusaidieni, au wanajisaidia wenyewe?
(94) Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu,
(95) Na majeshi ya Ibilisi yote.
(96) Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:
(97) Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhaahiri,
(98) Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.
(99) Na hawakutupoteza ila wale wakosefu.
(100) Basi hatuna waombezi.
(101) Wala rafiki wa dhati.
(102) Laiti tungeli pata kurejea tena tungeli kuwa katika Waumini.
(103) Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
(104) Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
(105) Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.
(106) Alipo waambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamchimngu?
(107) Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
(108) Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
(109) Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
(110) Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
(111) Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanao kufuata ni watu wa chini?
 


اتصل بنا | الملكية الفكرية DCMA | سياسة الخصوصية | Privacy Policy | قيوم المستخدم

آيــــات - القرآن الكريم


© 2022